Na Eliud Dalei,Geita 26/06/2014
Matukio ya ajabu yanayofanywa na mahabusu wanaoshinikiza kesi zao
kusikilizwa haraka ikiwa ni mbinu wanazoamini zitasaidia katika kile
wanachoeleza kuwa ni kudai haki zao yanaendelea kuonekana ambapo jana mahabusu Wilayani
Geita walifanya tukio la aina yake.
Mahabusu wanane wanaoshikiliwa kwa
tuhuma mbalimbali zikiwemo za mauaji jana wakati wakitoka mahakamani baada ya mashauri yao kuahirishwa waliung’ang’ania
mlingoti wa bendera ya Taifa huku wote wakivua nguo zote na kubaki mtupu.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa 3:15 hadi saa 4:15 asubuhi katika Mahakama ya Hakimu
Mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Geita.Mahabusu hao hao walivua nguo zote na kubaki mtupu na kisha kupiga kelele wakiwa wameshikilia mlingoti waakieleza kilio chao.
“Haiwezekani tangu mwaka jana tulipokamatwa hadi sasa kesi zetu zinapigwa
kalenda. Wengine tumebambikiwa kesi. Tunaomba haki zetu, polisi wanatuonea,
vyombo vya habari tunaomba mtusaidie tumekaa muda mrefu bila kusikilizwa na hatujui
hatma yetu tangu mwaka 203,tulipokamatwa. Tumechoka kukaa mahabusu, tunaomba
kesi zetu zisikilizwe.” Alisema Iliza Warioba mmoja wa mahabusu hao.
Waliovua
nguo na kung'ang'ania mlingoti,nje ya mahakama ya Mwanzo nyankumbu
ambayo kwa sasa inatumika kama ya wilaya baada ya ile ya wilaya kutumika
kama mahakama kuu ni pamoja na Iliza Warioba,Stephen James,Kalebu
Ochieng na Masha Joseph.
Wengine ni Omari Juma,Nicholaus Kisinza,Daud Lumumba,Gofrey Luta,Emanuel Daud na Saimon Panya.
Mkuu wa polisi wa wilaya ya Geita,Busee Bwire aliwataka watuhumiwa hao
waondoke katika mlingoti na kuvaa nguo ili waingie kwenye gari ili warudishwe
gerezani kwani kitendo walichokuwa wakikkifanya ni kosa la jinai lakini
waligoma..
“Pamoja na maamuzi yenu haya, lakini mtambue mnavunja sheria na hili ni kosa
jingine la jinai, hivyo ni vyema mkaondoka kwenye mlingoti huu na kuingia
kwenye gari Malalamiko yenu tumeyasikia na yatashughulikiwa.” Alisema Bwire
Hali hiyo,ilimlazimu Ocd Bwire
kuagiza askari wa kikosi cha kutuliza ghasia FFU na walipofika eneo hilo
la mahakama walitaka kuwatoa kwa nguvu kwenye mlinoti mahabusu hao
ambao walitishia kushusha bendera hiyo ya taifa iwapo askari yeyote
angewagusa.
''Tulishakufa tayari tukiwa
gerezani hivyo askari atakayetugusa hapa tuko tayari kufa
naye,tumeshachoka na ndiyo maana hapa tumeishika
serikali(mlingoti)tuanomba mtuache au aje mkuu wa mkoa na mwanasheria wa
serikali achukuwe kero zetu''walisikika mahabusu hao wakichimba mkwara.
Kufuatia hali hiyo,Katibu tawala
wa Wilaya ya Geita,Gasto Gaspari alifika eneo hilo akidai ameagizwa na
mkuu wa mkoa huo kuja kuwasikiliza malalamiko yao ambapo walimueleza
kila kitu na kuahidi kufikisha kilio chao kwa seriakaali.
Baadaye alikuja mwanashheria wa
serikali Hezron Mwasimba aliyewasihi wakubali kupanda kwenye gari na
kurudishwa gerezani huku akiwahakikishia majira ya saa saba jopo la
wanasheria,wakiwemo mahakimu na viongozi wa serikali kufika lilipo
gereza hilo kwa ajili ya kuzungumza na mahabusu wote wa gereza hilo.
Kumekuwepo na malalamiko ya muda
mrefu kutoka kwa mahabusu wakilalamikia kesi zao kuchukua muda mrefu na
hata wanaponyoosha mikono kuwaeleza mahakimu wamekuwa wakidai
kutosikilizwa.
MWISHO
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni