Jumanne, 14 Julai 2015

WATAKIWA KUIMBA UKAWA KWANZA MAGUFULI BAADAYE!

Na Victor Bariety,Geita 14/07/2015

SIKU chache baada ya CCM kumpitisha Dk John Magufuli kuwa mgombea wake wa urais,baadhi  ya wananchi wa wilaya ya Geita Mkoa wa Geita na viongozi wa CHADEMA wamewataka watanzania kwa ujumla kutembea wakiimba Ukawa  kwanza Magufuli baadaye kwa kile walichodai mgombea  huyo wa urais kupitia chama cha hicho anayetoka mkoani hapa hana jipya kwani hawezi kulketa  mabadiriko yoyote.


Upendo Peneza akihutubia wakazi wa mji wa Geita katika viwanja vya stand ya zamani


Kutokana na hilo wananchi hao wamewataka watanzania kuunga mkono vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi(UKAWA),kwa kuchagua rais,mbunge na diwani anayetokana na umoja huo kwani ndiyo tumaini ambalo litaleta mabadiriko ya kweli katika kuinua uchumi na kuwafanya watanzania wafaidi raslimali zao ambazo kwa miaka mingi zimekuwa zikiishia mifukoni mwa mafisadi wachache.

Wananchi hao walikuwa wakitoa maoni yao baada ya kupewa fursa ya kuuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ulioitishwa na mjumbe wa mkutano mkuu BAWACHA Taifa Upendo Peneza ambaye pia ni mtia nia wa ubunge wa jimbo la Geita kupitia chama cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA)uliofanyika jana(juzi)uwanja wa stand ya zamani  ya mjini Geita.

‘’Mimi sijasimama hapa kuuliza swali,kwanza nikupongeze kwa hotuba yako nzuri ila mimi nilikuwa nashauri watanzania wenzangu hususani wanaotoka katika mkoa wa Geita  msije mkabweteka chama cha mapinduzi  kuwateulia mgombea wa urais kutoka kwenu na ninataka niwaeleze tu kwamba ndani ya chama cha mapinduzi(CCM), hata akisimamishwa maraika tusitegemee mabadiriko yoyote’’

‘’Mnachotakiwa kufanya kila  mmoja wenu atembee akiimba wimbo wa ukawa kwanza Magufuli baadaye na ndiyo njia pekee itakayopelekea kuondokana na umaskini unaotukabili maana kama ameshatamka hadharani kwamba hatawaangusha na atailinda ilani ya CCM,mnategemea nini hapo kwamba wezi atawalinda maana ndiyo sera ya chama chao’’alisema Yukuri Yukuri huku akishangiliwa.

Kwa upande wake Peneza aliwataka wakazi wa jimbo la Geita kumuombea dua ili chama chake kimteuwe kwenye kura za maoni  na baadaye kuwa mbunge wa jimbo hilo ili alete mabadiriko ambayo yamekosekana chini ya wabunge wa chama cha mapinduzi(CCM).

‘’Iwapo nitachaguliwa kwenye kinyang’anyiro hicho nitahakikisha uongozi wangu ni wa vitendo zaidi siyo wa maneno maana kero zote zinazowakabili wanageita ni kutokana na makosa ambayo mmekuwa mkiyafanya kila baada ya miaka mitano kwa kuchagua wabunge wa CCM,huduma za afya mbovu,hakuna maji,wachimbaji hawana maeneo na wanapoibua dhahabu wanafukuzwa,nitahakikisha hayo matatizo yanabaki historia ninaomba dua zenu ili chama kiniteuwe na niwe mbunge wenu’’alisema Peneza huku akishangiliwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni