Alhamisi, 2 Julai 2015

SANGOMA AKIMBILIA KANISANI AKIWAKWEPA POLISI

Na Victor Bariety,Geita 
Wakati Taasisi,mashirika,ya serikali na binafsi yakipiga vita ramli chonganishi zinazosababisha mauaji ya vikongwe na albino,Mganga wa kienyeji ameamua kujisalimisha katika kanisa la TAG na vifaa vyake kuteketezwa kwa moto na viongozi wa kanisa hilo.

                                                   mchungaji akiteketeza tunguri za mganga
 
Mganga huyo,Luhanga Mkakazi(70)mkazi wa Mtaa wa Mwatulole mjini Geita amejisalimisha jana(Jumamosi)katika kanisa la TAG lililopo jirani na nyumbani kwake baada ya kukerwa na shughuli za uganga kuhusishwa na mauaji ya vikongwe na walemavu wa ngozi(Albino).
Uamuzi wa mganga huyo umekuja siku moja tu baada ya walemavu wa ngozi kuadhimisha siku ya Albino duniani ambapo hapa nchini shughuli hizo zilifanyika jijini Arusha na mgeni rasmi alikuwa Rais Dk.Jakaya Kikwete.
Aidha akizungumza katika Ibada Maalumu ya kanisa hilo,Mkakazi amesema,ameamua kuachana na uganga na kumrudia mwenyezi Mungu huku akidai kukerwa na shughuli hizo kuhusishwa na imani za kishirikina zinazosababisha mauaji ya Albino na Vikongwe.
Amesema alianza shughuli za Uganga akiwa na umri wa miaka 34 kwa kutibu magonjwa mbalimbali pamoja na kupiga ramli ili kutambua matatizo ya wateja wake ambao wengine walikuwa wakifika kwake kutafuta dawa za biashara.
Mchungaji wa TAG Sanyajuu mjini Moshi Alfredy Mtinda  ambaye alikuwa akiongoza ibada ya kumuombea mganga huyo amesema vifaa vilivyoteketezwa ni pamoja na ungo,shanga,vibuyu vya dawa na nguo za sughuli za uganga,huku akiwaomba viongozi wengine wa dini kueneza injili na kuwaelimisha watu kuachana na uganga wa kienyeji.
Mwinjilisti wa kanisa hilo,Samweli Magazi amesema tukio linaifundisha jamii kuachana na imani potofu za kutumia viungo vya albino na badala yake kumwamini Mungu.
Katika mkoa wa Geita,takwimu zinaonyesha kuwa tangu mwaka 2007 walemavu wa ngozi(Albino) sita wameuawa,watatu wakijeruhiwa huku  vikongwe waliouawa katika kipindi cha Mwaka jana ni
Mwisho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni