Jumapili, 30 Agosti 2015

MWANAJESHI MBARONI KWA MAUAJI GEITA

Jeshi la polisi Mkoani Geita limemkamata mstaaf wa jeshi la wananchi Tanzania kikosi cha Komando sajent Mathias Christopher  Etta(55)kwa tuhuma za mauaji ya mchimbaji mdogo wa madini ya dhahabu.

Etta pia ni msimamizi msaidizi wa kampuni ya ulinzi ya (Nguvu moja security service) inayofanya shughuli zake za ulinzi kwenye mgodi wa madini wa Bacreef uliopo maeneo ya Lwamgasa mkoani hapa.

Sajent Etta alitiwa nguvuni jana majira ya saa 8 mchana kwenye kituo kidogo cha polisi cha Bacreef baada ya mwili wa  marehemu Yona Onesmo (35) ambae ni mkazi wa kijiji cha Isingiro kata ya Lwamgasa na mchimbaji mdogo kukutwa umetupwa pembezoni mwa barabara karibu na daraja la kijiji cha Mnekezi umbali wa kilomita  (2) kutoka  Lwamgasa na kilomita takribani  (15)kutoka Hospitali ya Katoro alikokua amepelekwa kupatiwa matibabu.

Imeelezwa na mashuhuda wa tukio hilo kuwa,baada ya  kupigwa usiku wa kuamkia julai 30 mwaka huu na walinzi wa kampuni ya( Nguvu moja) kwa kosa la kukutwa wanachimba kwenye eneo lililozuiliwa la mgodi wa Bacreef alikimbizwa hospitalini kabla ya mwili wake kukutwa pembezoni mwa Barabara itokayo Katoro kwenda Lwamgasa  majira ya saa nne asubuhi baada ya wakazi wa kijiji cha Mnekezi kupewa taarifa na wapita njia ukiwa bado una (Kanyura) za Hospitali zinazotumika  kutundikia drip za maji.

 “Kiukweli Katoro  kwenda kutibiwa”alisema afande Samweli Yusuph wa kituo hicho  aliyeutambua mwili huo baada ya kufika eneo la tukio.nashangaa amefikafikaje hapa kwani jana mimi nimewapeleka Hospitali ya

 Mganga mkuu wa Hospitali ya Katoro Dk Daniel Izengo alionyesha kushangazwa na taarifa  hiyo kwani alikua bado hajapokea taarifa yakupotea kwa mgonjwa hospitalini hapo,licha ya ( postmotam)yaani kikao cha wafanyakazi wa hospitali hiyo kuwa tayari kilikuwa kimeshafanyika.

Hali hiyo ilimlazimu Dk,Izengo kumtafuta mhudumu aliyekuwa zamu Dk,David Mgalula ili kuzungumzia kizungumkuti hicho,akitolea ufafanuzi mhudumu huyo alikili kuwapokea wagonjwa hao wawili Bwana (Onesmo na Ndagicheye) nakusema kuwa hali ya Bw,Onesmo haikuwa nzuri kwani Marehemu alidai kuwa anajisikia maumivu makali tumboni.

“Nikweli niliwafanyia uchunguzi wa awali (Physcal chekup)nikabaini walikua na michubuko mikononi,usoni pia walikua  wamevimba joint ila marehemu alidai kuwa tumbo linamuuma nilimwandikia sindano za masaa 6 aina ya(X-pen) Sindano za Tetenasi na dawa zakumeza aina ya (Dicrofenaki)kila baada ya masaa 8 pamoja na drip,mwenzake aliruhusiwa kwani alikua anajisikia vizuri,sasa nashangaa kwanini marehem aliamua kutoroka,labda alihofia kushitakiwa na Mgodi wa Bacreef”alisema Dk huyo.

Kwa upande wa Sajent Hamis Kabonga ambaye ni msimamizi mkuu wa kampuni ya ulinzi ya (Nguvu moja security service ) alikiri kushikiliwa kwa msaidizi wake nakuongeza kuwa kukamatwa kwake kunatoka na utata wa kifo cha Yona onesmo ambae alikua nimiongoni mwa watuhumiwa waliokamatwa julai 30 saa 11 kwa ajili ya  kufikishwa mahakamani mara baada yakutibiwa.

Hata hivyo hakuwa tayari kuzungumzia uwepo wa migogoro ya mara kwa mara kati ya kampuni hiyo ya uchimbaji ya Bacreef na wananchi wanaozunguka mgodi huo kwa madai kuwa msemaji wa kampuni hiyo yuko safarini hadi pale atakaporejea.

Aidha uchunguzii wa gazeti hili umebaini kuwa,licha ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Geita kukutana na pande hizo mbili mwanzoni mwa mwaka huu kati ya April na Mei mwaka huu ili kutatua migogoro hiyo,bado matukio yenye utata yanaendelea kujitokeza mgodini hapo.

Kwa upande wake kaimu kamanda wa polisi Mkoani Geita,Peter Kakamba amethibitisha kushikiliwa kwa mstaaf huyo wa jeshi la wananchi Tanzania  kwa mahojiano zaidi.

MWISHO.                      

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni