NA VICTOR BARIETY,GEITA
Wagombea saba wa kura za maoni ndani ya Chama cha Mapinduzi
wamepinga matokeo ya uchaguzi kwa madai kwamba yamegubikwa rafu na karatasi za
kupigia kura kutokuwa na picha za wagombea huku wakitishia kufanya maamuzi magumu iwapo malalamiko yao yatapuuzwa.
Pia
wamedai kwamba jina la mgombea mmoja la Juma Malunga ambaye alijitoa katika
kinyang’anyiro jina lake likikuwepo katika karatasi za kupigia kura na kupata
kura 184 ambaye hata hakupiga kampeni.
Wagombea
walijitokeza kupinga matokeo hayo na kura zao katika mabano ni Paschali
Malugu(2,253)ambaye amekuwa wa pili mbele ya Contantine Kanyasu aliyetangazwa
mshindi kwa kura 2,553.
Wengine
ni Jacob Mtalitinya(1,249),Evarist Nyororo(1,187),Dk.Lonard
Mugema(410),Dk.Daffa Mohamed(213) ,Juma Malunga(184),Seif Kulunge(158),Regina
Mikenzi(251),na Dk Samweli Opurukwa(218).
Aidha
wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi huo,Mkurugenzi wa Uchaguzi CCM wilaya ya
Geita,Kilian Balindo katia ya watia nia 10 waliojitokeza kwenye mkutano wa
kutangaza matokeo hayo walikuwa watatu tu,Mikenzi na Merikiory pamoja na
Kanyasu,huku idadi ya wanachama wa CCM waliojitokeza kusikiliza wakiwa wachache
sana.
Akizungumza
kwa niaba ya watia nia wenzake,Dk.Opurukwa alisema wanapinga matokeo hayo kwa
kutokana na Zoezi zima la upigaji wa kura za maoni Agosti Mosi kukubigwa na
rafua za rushwa na baadhi ya viongozi kuwapigia debe baadhi ya wagombea.
“
kwanza karatasi hazikuwa na ubora,tulitarajia kuwa na picha za
wagombea,karatasi zilikuwa hazina picha,wagombea tuliokuwa tunafahamika
tulikuwa kumi,lakini wagombea waliojitokea 11,wagombea wawili majina yao
yanafafana kwa karibu sana ambapo kufanana kwa majina hayo yanawezea
kuwachanganyanya wapiga kura”alisema Dk.Opurukwa.
Alisema
dosari zingine zilijitokeza katika Kata ya Mugusu ambako kulitakiwa kuwa na
wapiga kura 300 lakini walkiojitokeza kupiga kura walikuwa 747 na
Tawi la Machinjio wapiga kura walikuwa 300 waliopiga kura 350.
“Dosari
zingine ni kadi za wana ccm zilizokuwa zinatakiwa kupigiwa kura hazikuwa
na picha na zingine zilikuwa hazijalipiwa ada”alisema msemaji wa watia nia hao.
“Kata
ya Bung,wangoko,Bulela mambo hayo yalijitokeza sana,Dosari ya tano katika
kufanya majumuisho kutoka kwenye vituo,hakukuwa na wawakilishi wa
wagombea,dosari nyingine mmoja wa wagombea aliweza kuweka bango lenye picha
yake na picha ya mgombea wa CCM kwa nafasi ya Urais”alisema Dk.Mugema
“Kwa
maana ya kwamba mgombea huyo alikuwa ametumwa na mgombea urais,ambapo aliweka
mabango sehemu mbalimbali akiwaaminisha kwamba yeye ndiyo mgombea pekee na
anayefaa.
Alisema
kwa ushahidi walioupata baadhi ya viongozi wa chama walikuwa wakimpigia
debe mgombea mmoja,Tumeandika barua yetu tunasubiri”.
Wagombea
hao wameandika barua kwenda kwa mkurugenzi wa Uchaguzi na nakala kwa ofisi ya
mkoa na makao makuu ya CCM Taifa.
Akizungumzia
malalamiko ya wagombea hayo Mkurugenzi wa Uchaguzi alisema katika zoezi la
uchaguzi hakuna dosari iliyojitokeza.
Alisema
malalamiko yao hayana ukweli wowote na kwamba hakuna barua walioyoipokea kutoka
wa wagombea hao.
“Mimi
sijapata malalamiko,hadi natangaza matokeo muda huu hakuna barua iliyotumwa ya
kulalamika”alisema Balongo.
Matokeo
katika jimbo la Geita Vijijni,aliyeshindwa Joseph Msukuma 9,699,Ernest
Mabina(1,501),Thomas Ntogwakulya 811,Pima Marko 461 ,Luponya Sherembi 408,na
Sabato Vitusi(107).
Busanda
aliyeshinda Lolesia Bukwimba kwa kura 13817,Tumaini Magesa kura 6363,Sostenes
Kulwa 1858,Fransic Kiganga 1150,Luchenhe Mbatilo 134,na Mhonzu John 117,na
Malembeka Mark 96.
Jimbo
la Chato,aliyemridhi Dk.John Magufuli ni Dk.Merdadi Kalemani 12,892,Deusdedit
Joseph 3,251,Simon Michael 2,150,Dk.Alphonce Chandika 1,244,Revocatus Alex
661,Luge Ismail 539,Aman Shaaban 538,Majura Kasika 369,Michael Jigabha
348,Mkinga Mkinga 321 na Yohana Nasorro 111.
Mwisho.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni