NA VICTOR BARIETY,GEITA
MAKAMU wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilal, amewataka waislam
na watanzania kwa ujumla kuhakikisha wanadumisha amani na umoja ulioachwa na
waasisi wa taifa hili hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu.
Dkt. Bilal aliyasema hayo
jana katika Hotuba yake aliyoitoa katika Baraza la Idd lililofanyika kwenye ukumbi wa Shule ya sekondari ya wasichana
Nyankumbu iliyopo mjini Geita.
Alisema tangu Karne
zilizopita Tanzania pamekuwa pahala pa amani
na utulivu na hivyo kuitaka jamii kutoa ushirikiano wa hali ya juu kwa vyombo
vya ulinzi na usalama ili kuwafichua watu ambao wanaoharibu amani iliyopo.
Dkt. Bilal alisisitiza kwamba, amani ni msingi pekee katika taifa kujiletea
maendeleo, ambapo alisema bila amani
maendeleo hayawezi kupatikana kwani watu hawatafanya kazi kwa uhuru unao
hitajika.
‘’Kiujumla hali ya amani
na utulivu imetanda kote katika Mikoa ya Tanzania hali inayopelekea Serikali
kupanga na kutekeleza mipango yake ya kimaendeleo kwa lengo la kuimarisha uchumi
na ustawi wa Wananchi wake sasa naomba kusisitiza amani tuliyo nayo iendelee
kudumu pia nawaomba waumini wote mdumishe umoja huu tulionao ili tuweze kusonga
mbele,alisema dkt. Bilal.
Mbali na kutoa wito huo Dk. Bilal alilaani mauaji yaliyotokea nchini Burundi na kuwataka viongozi wote
duniani kukaa na kujadili namna ya kurejesha amani hiyo.
Awali Mkuu wa Mkoa
wa Geita Fatuma Mwassa alimpongeza Dkt. Bilal kwa uongozi wake mzuri katika
kipindi cha awamu ya nne, chini ya Rais
wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete kwani wamefanya mengi nchini likiwemo suala la
uhuru wa watu kujieleza na kutoa maoni yao.
“Nakupongeza sana kwa uongozi wako katika kipindi cha awamu ya nne chini ya rais
wetu Dkt. Jakaya Kikwete, mmefanya mengi hasa katika Mkoa wetu wa Geita na
Tanzania kwa ujumla na kwa niaba ya wananchi wa Geita tunawashukuru kutupatia
mgombea urais kutoka Mkoa wetu wa Geita Mh. John Magufuli,’’alisema Mwassa.
Naye katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Sheikh Suleiman Lolila aliwataka waislam na watanzania kwa
ujumla wenye vigezo vya kupiga kura wajitokeze kwa wingi kwenda kupiga kura
pindi zoezi hilo litakapowadia Oktoba 25 mwaka huu.
MWISHO.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni