Na Eliud Dalei,Geita 16/09/2014
ASKARI
mgambo wawili wa kituo cha polisi cha Nzera kilichopo Tarafa ya Bugando
Wilayani Geita Mkoa wa Geita wamefanya unyama wa kutisha baada ya kumshambulia
kwa kipigo mwalimu msitaafu kisha kumvunja mbavu zake kabla ya kumtembeza mtaani
akiwa uchi wa mnyama.
Mgambo
wanaotuhumiwa kufanya unyama huo wanadaiwa kushirikiana na watu wawili ndugu
waliotajwa kwa majina ya Masalu Mwanangwa na Kona Mwanangwa wote
wakazi wa kijiji hicho cha Nzera.
Tukio
hilo limetokea Septemba 14 mwaka huu majira saa 3 asubuhi wakati majeruhi Mwalimu
Samsoni Mzingwa(58),akielekea shambani kwake.
Akiongea
na waandishi wa habari hizi katika hospitali ya Wilaya ya Geita kwenye wodi
namba 8 alikolazwa, Mwalimu
Mzingwa
alidai kuwa siku ya tukio alishutukia watu wanne wakiwa na mgambo wawili wa
kituo hicho cha polis Nzera kisha kumzingira na kuanza kushushia kipigo kikubwa hali iliyopelekea kupoteza
fahamu.
Amesema
kana kwamba hiyo haitoshi,walipomaliza kumpiga walimvua nguo zote na kuanza
kumtembeza akiwa uchi wa mnyama kabla ya kuokolewa na wananchi wa eneo hilo
waliomchukua hadi katika kituo cha afya cha Nzera na baadaye alikimbizwa kwenye
hospitali ya wilaya ya Geita kutokana na hali yake kuwa mbaya ambako amelazwa
hadi sasa.
Amefafanua
kuwa,pamoja na kuwatambua waliomfanyia kitendo hicho hakuna hatua
zilizochukuliwa dhidi ya wahusika ambao wanaendelea kutamba.
Akifafanua
Chanzo cha yeye kupigwa,mwalimu Mzingwa amesema,alikodiswa shamba mwezi huu kwa ajili ya kulima
Maindi na watu aliowataja kwa majina ya Rukasi Bunzali pamoja na Wiliamu
Bunzali wote wakiwa ni wanafamilia moja kwa makubaliano ya kuwalipa kiasi cha
shilingi milioni moja na laki tano ambapo aliwalipa pesa zote na kuanza
kulima kwa ajili ya kupanda mazao.
‘’Majuzi wakati
nikienda shambani kwangu nilishutukia watu wanne wakiwa na mgambo wawili wa
kituo cha polis Nzera kambao walinizingira na kuanza kushushia kipigo kikubwa
hadi wakanivunja mbavu huku wakinitembeza uchi wa mnyama lakini wananchi
waliniokoa na nilikuja kujikuta nipo hapa hospitalini nimelazwa’’alisema
Mzingwa kwa taabu.
Kwa
upande wake mtoto wa mzee huyo Baraka
Samsoni amesema baada ya kupata taarifa za kujeruhiwa baba yake alikwenda
kujiridhisha na baadaye alitoa taarifa
kwa OCS Nzera lakini hakuna kilichofanyika zaidi ya kutishwa huku akiambiwa
asiwafundishe kazi.
Mganga
mfawidhi wa Hoaptali ya Wilaya ya Geita Dk Adam Sijaona amekiri mgonjwa huyo
kuvunjwa mbavu kutokana na uchunguzi wa awali waliomfanyia.
Mtendaji wa kijiji cha Nzera Henry mapembegamva
amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo alilodai kiini chake ni mgogoro wa ardhi.
Kamanada
wa polisi Mkoani Geita Josefu Konyo alipopigiwa sm yake ya kiganjani hakupokea
na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa maandishi hakujibu.
MWISHO
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni