Na Eliud Dalei,Geita 1109/2014
Miili ya Watoto watatu wa familia moja waliofariki dunia baada kuteketea kwa moto ndani ya nyumba waliyokuwa wamelala katika Mtaa wa Elimu Nyankumbu mjini Geita imezikwa Nyumbani huku simazi,vilio na majonzi vikitawala nyumbani kwa familia hiyo.
Miili
ya watoto hao,Reginard Robert(9) Mwanafunzi wa darasa la Pili shule ya
msingi Nyankumbu,Sophia Robert(6) wa darasa la awali,na Lemijonsi
Robert(4)ilizikwa juzi saa 11:30 jioni nyumbani kwao.
Watoto
hao waliteketea kwa moto saa 8 usiku wa kuamkia juzi baada ya mtu
anayedaiwa kuwa na ugomvi na familia hiyo unaotokana na kugombania eneo
la kufyatulia matofari kuiteketeza kwa moto Nyumba hiyo baada ya
kuimwagia mafuta ya petroli.
Mazishi hayo yalihudhuliwa na viongozi mbalimbali wa serikali,dini na wananchi wa maeneo mbalimbali ya mji wa Geita na kuzikwa kwa heshima zote.
Wakati
mazishi hayo yakifanyika baba mzazi wa watoto hao,Robert
Reginard(49)alionekana kuishiwa nguvu kabisa mbali ya kuwa na majeraha
ya kuungua moto kichwani,kilichomuumiza zaidi ni kupotelewa na watoto
wake watatu na mmoja akiwa na hali mbaya hospitalini.
Mganga
mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya Geita,Dk.Adamu Sijaona alisema hali
za wazazi wa watoto hao,akiwemo mama yao Angelina Gaspar(38) wanaendelea
vizuri isipokuwa binti yao,Scholastika Amos(16) alipelekwa katika
hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa matibabu zaidi kutokana na hali yake
kuwa mbaya.
Dk.Sijaona
alisema mtoto huyo alikimbizwa Bugando saa 4 asubuhi na gari la
kubeba wagonjwa(Ambulance),kutokana na hospitali hiyo ya wilaya kutokuwa
na vifaa maalumu vya matibabu kulingana na majeraha ya moto aliyokuwa
nayo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni