Na Eliud Dalei,wa goldzoneblog Geita
15/09/2014
Ofisa
mazingira wa Halmashauri ya wilaya ya Geita,Hellen Eustace amejikuta
kwenye wakati mgumu,baada ya kuzomewa na wananchi wa kijiji cha
Nyarugusu wilayani hapa,kwenye mkutano wa Hadhara wa mwenyekiti wa Chama
cha Mapinduzi(CCM),Mkoa wa Geita,Joseph Musukuma kufuatia na uchafuzi
wa mazingira wa vyanzo vya maji unaotokana na utitiri wa viwanda vya
kuchakata mchanga wa Dhahabu.
Eustace
alijikuta katika hali hiyo,baada ya kutakiwa na Mwenyekiti
Musukuma,kujibu malalamiko ya muda mrefu ya wakazi wa Kijiji hicho
yanayotokana na viwanda hivyo kutiririsha maji machafu ya kemikali ya Zebaki ambayo huingia kwenye vyanzo vya maji.
Hatua
hiyo ilitokana na Malalamiko yaliyotolewa na wananchi kwenye mkutano
huo,ambao walidai kwamba Uchafuzi huo umewafanya kuishi kwa hofu kuhusu
Afya zao kutokana na Kijiji hicho kuzungukwa na viwanda vingi ambavyo
hutiririsha maji hayo kwenye vyanzo vya maji wanayotumia kunywa,na
matumizi mengine ya Nyumbani.
Mmoja
wa wananchi hao,Vicenti Mukoma,alidai kuwa wamekuwa wakiishi kwa
mashaka kwani kemikali hizo ni hatari kwa Afya za Binadamu na wanayama
wengine wakiwemo mifugo na hivyo kumuomba mwenyekiti wa CCM kuchukua
hatua juu ya tatizo hilo.
“Mwenyekiti,Nyarugusu
inazungukwa na Viwanda vingi sana vya kuchenjua Maludio,na maji
yanayotoka kwenye viwanda hivyo yanaingia kwenye vyanzo vya maji
tunavyovitegema siku zote,sasa hali hii inatuadhiri Afya zetu”alisema
Mukoma.
Baada ya
Malalamiko hayo,Mwenyekiti wa CCM aliyekuwa ameambatana na Watumishi wa
Halmashauri ya Geita,akiwemo kaimu mganga mkuu,Dk.George Rweyemela,na
watumishi wa Nyarugusu,alimtaka Ofisa mazingira kujibu malalamiko hayo
mbele ya mamia ya wananchi waliokuwa wamefurika kwenye mkutano huo.
Katika
hali ya kushangaza Ofisa mazingira alijikuta akiambulia kuzomewa baada
ya kukiri kuwa kweli shughuli za uchimbaji wa madini na uchenjuaji wa
dhahabu unaharibu mazingira huku akidai kwamba suala hilo
linashughulikiwa na ofisi yake.
“Mwenyekiti
ni kweli mazingira yanaharibika,na shughuli zote za uchimbaji hata kule
Ng’hwag’alanga mnaharibu mazingira labda tupafunge”alisema hali
iliyowafanya wananchi kupinga kauli hiyo na kuanza kumzomea wakimtaka
afute kauli yake kwa kuwa kinachoharibu vyanzo vya maji ni Viwanda vya
kuchenjua mchanga wa dhahabu na sio machimbo ya wachimbaji wadogo.
Baada
ya zomea zomea hiyo,mwenyekiti wa CCM alimtaka kujibu kilichoulizwa na
wananchi kuhusu Viwanda hivyo badala ya kuzungumzia machimbo ya
wachimbaji wadogo na ndipo alidai kwamba suala hilo linashughulikiwa na
ofisi yake.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni