Alhamisi, 2 Julai 2015

WATU 227 WALIPOTIWA KUUGUA UGONJWA WA KIFUA KIKUU

NA VICTOR BARIETY,GEITA 02/07/2015
Watu 227 wameripotiwa kuugua ugonjwa wa Kifua Kikuu mwaka 2012/13 kwenye Maeneo ya Migodi ya wachimbaji wadogo katika wilaya za Kahama mkoani Shinyanga na Geita mkoani Geita.

                                                  Mwandishi Victor Bariety akiwa kazini

Takwimu hizo zinatokana na Utafti ulifanywa Mwishoni mwa mwaka jana kwa kushirikisha wadau wa Afya likiwemo shirika la Kimataifa la Uhamiaji(Internation Organization For Migration -IOM),wachimbaji wadogo na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Taarifa ya Utafti huo iliwasilishwa jana(Alhamisi) kwenye mkutano mkuu wa Wadau hao uliofanyika jijini Mwanza ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa azimio la nchi za Kusini mwa Afrika SADC la kuthibiti ugonjwa wa kifua kikuu kwenye maeneo ya Migodi.

Akiwasilisha taarifa ya utafti uliofanyika kwenye migodi ya Kalole na Mwaziba wilayani Kahama Mshauri wa Afya wa Mgodi wa ACCACIA Dk.Zumbe Musiba alisema,kuwa watu 54 wameripotiwa kuugua ugonjwa wa Kifua kikuu(TB)katika maeneo hayo.

Alisema watu hao wameripitiwa kuugua TB baada ya kufikishwa kwenye vituo vya Afya vya kata za Lunguya na Chela kupima Afya zao kutokana na kuishi katika migodi ambayo mazingira yake ni machafu yenye vumbi kali na matumizi ya zebaki bila kuwa na tahadhari.

Dk.Musiba alisema asilimia 50 ya kesi za Ugonjwa wa Kifua kikuu zilizoripotiwa katika maeneo hayo zina uhusiano mkubwa na Maambukizi ya Virusi vya Ugonjwa wa Ukimwi.

"Kati ya watu tuliowahoji,Utafti unaonyesha kuwa wengi hawajui dalili za TB hata viongozi wao hawajui dalili na chanzo cha Ugonjwa huo,Tumeona chanzo cha ugonjwa huo ni mwingiliano mkubwa wa watu,Vumbi linalotokana na uzalishaji wa mawe ya dhahabu,Nyumba finyu zisizopitisha hewa"alisema Dk.Musiba.

Aidha Mratibu wa mpango wa Taifa wa Kuthibiti Kifua Kikuu  na Ukoma Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Dk.Alln Tarimo amesem katika Mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi ya Gold Crest kwamba katika utafti uliofanyika Katika Migodi miwili ya Nyakagwe na Mgusu wilayani Geita unaonyesha watu 172 wameripotiwa kuugua TB.

Alisema katika Mgodi wa Nyakagwe watu 63 waligundulika kuwa na Ugonja wa TB Mwaka 2012 na mwaka 2013 walioripotiwa kuugua ugonjwa huo ni watu 62.

Dk.Tarimo aliongeza kuwa katika Mgodi wa Mgusu waliogundulika kuwa na TB mwaka 2012 ni watu 17,na idadi hiyo iliongezeka hadi kwa mwaka 2013 ambapo waliogungulika kuwa na ugonjwa huo ni watu 30.

Hata hivyo alifafanua kuwa pamoja na Nyakagwe kuwa na kituo cha Afya hakina huduma ya Kupima ugonjwa wa Kifua Kikuu na hivyo wanannchi hutembea umbali wa kilomita 25 kwenda kituo cha Afya Bukoli.

"Tulipofika Mgusu hapakuwa na kituo cha Afya wala huduma ya Vyoo hakuna hatua hiyo huwalazimu wananchi wa maeneo hayo kusafiri umbali wa kilomita 23 hadi 25 kwenda kupata tiba hiyo kwenye Hospitali ya wilaya ya Geita na Kituo cha Afya Nyankumbu"alisema Tarimo.

Mganga Mkuu wa wilaya ya Geita,Dk.Noel Makuza alisema serikali kupitia idara ya Afya wilaya haijapeleka huduma ya Kituo cha Afya katika kijiji cha Mgusu chenye wachimbaji 9,324 kutokana na kijiji hicho kutotambuliwa.

Alisema Mgusu ni kijiji ambacho hakijasajiliwa na kwa kuwa serikali ipo kwenye mchakato wa kukisajili kitapata huduma stahiki zinazotolewa na serikali ikiwemo huduma ya Afya.

Kwa upande wake Naibu meneja wa mpango wa Taifa wa Kuthibiti kifua Kikuu Wizara ya Afya Dk.Liberate Mleoh,alisema Mpango huo unalenga kufikia malengo ya Taifa ya kuwa na wagonjwa sifuri wa TB ifikapo mwaka 2035 kutekeleza azimio la nchi za Kusini mwa Afrika SADC la kuthibiti ugonjwa huo kwenye maeneo ya Migodi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni